1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Herzog ataka dunia ipinge chuki dhidi ya Wayahudi

21 Desemba 2025

Kumbukizi ya tukio la mauaji ya Bondi, yafanyika chini ya ulinzi mkali nchini Australia

Rais wa Israel  Isaac Herzog  atowa mwito ulimwengu upambane na chuki dhidi ya Wayahudi
Rais wa Israel Isaac Herzog atowa mwito ulimwengu upambane na chuki dhidi ya WayahudiPicha: Abir Sultan/REUTERS

Rais wa Israel Issac Herzog ametowa mwito wa kufanyika kampeini duniani ya kupinga chuki dhidi ya Wayahudi.

Amesema hayo ikiwa ni wiki moja baada ya kutokea shambulio lililolenga tamasha la sikukuu ya wayahudi katika ufukwe wa Bondi nchini Australia, ambako watu 15 waliuwawa, wengi wakiwa wayahudi.

Kumbukizi ya shambulizi la ufyetuaji risasi katika ufukwe wa Bondi wiki moja iliyopitaPicha: Saeed Khan/AFP

Viongozi wa dunia walaani kwa hasira shambulio la risasi Bondi Beach

Wito wa kiongozi huyo wa Israel, ameutowa wakati maelfu ya waombolezaji wakikusanyika katika ufukwe wa Bondi chini ya ulinzi mkali, hivi leo kukumbuka tukio hilo la mashambulizi yaliyofanywa na watu wawili waliokuwa na bunduki.

Chuki dhidi ya Wayahudi

Viongozi mbali mbali wameshiriki kumbukumbu hizo akiwemo waziri mkuu wa Australia Anthony Albanese. Herzog ameyaomba mataifa ya ulimwengu kuchukuwa hatua kali na madhubuti na kuonesha uongozi imara katika kupambana na chuki dhidi ya Wayahudi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW