Migogoro
Trump: Vita vya Iran vinaweza kudumu kwa wiki kadhaa
3 Machi 2026
Matangazo
Ameyasema hayo mjini Washington katika hotuba yake ya kwanza tangu vita vya Israel na Marekani dhidi ya Iran vilipoanza.
Hayo yanajiri wakati ambapo Iran na washirika wake imeendelea kujibu mashambulizi dhidi ya Israel na katika nchi jirani za Ghuba.
Mashambulizi dhidi ya balozi za Marekani nchi za Ghuba
Mapema Jumanne imeushambulia ubalozi wa Marekani nchini Saudi Arabia kwa ndege mbili zisizo na rubani. Shambulio ambalo limefanywa baada ya kuulenga ubalozi mwingine wa Marekani nchini Kuwait Jumatatu.