1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Mexico aahidi utulivu ufunguzi wa Kombe la Dunia

9 Juni 2026

Rais Claudia Sheinbaum wa Mexico ametoa hakikisho la kuwepo utulivu wakati wa mechi ya ufunguzi wa Kombe la Dunia baadae wiki hii, licha ya wasiwasi kutokana na maandamano yanayoendelea.

Mexico City 2026 | Taswira kuelekea Kombe la Dunia
Taswira kuelekea Kombe la Dunia ambalo ufunguzi wake utafanyika kwenye mji mkuu wa Mexico. Picha: Gerardo Vieyra/NurPhoto/picture alliance

Muungano wa walimu nchini humo umetishia kufanya maandamano makubwa kwenye mechi ya ufunguzi kati ya Mexico na Afrika Kusini itakayofanyika kwenye mji mkuu, Mexico City ikiwa serikali haitotimiza madai yao ya nyongeza za mishahara na pensheni.

Kwenye mkutano wake wa kila siku na waandishi habari, Bibi Sheinbaum amesema serikali yake itahakikisha sherehe za Kombe la Dunia zinafanyika katika mazingira ya amani na utulivu.

Wiki iliyopita, polisi iliwatawanya waandamanaji kwa mabomu ya machozi na risasi za mpira nje ya uwanja mkubwa wa Zocalo ambao umetengwa kwa mashabiki wasiokwenda uwanjani, kutizama mechi kupitia televisheni.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW