1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Al-sisi afanya ziara ya kwanza Uturuki tangu achaguliwe

4 Septemba 2024

Hii ni ziara ya kwanza ya Rais Abdel-Fattah al-Sisi nchini Uturuki tangu kuchaguliwa kuiongoza Misri mwaka 2014, baada ya kuupindua utawala wa Rais Mohammad Mursi, aliechaguliwa kidemokrasia.

Rais wa Uturuki Erdogan na mwenzake wa Misri Abdel-Fattah al-Sisi.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na mwenzake wa Misri Abdel-Fattah al-Sisi wakisalimiana.Picha: Turkish Presidency/AP/dpa/picture alliance

Rais wa Misri, Abdel Fattah al-Sisi atafanya mazungumzo na rais Tayyip Erdogan nchini Uturuki leo ambako anafanya ziara yake ya kwanza, tangu miaka 12 kama kiongozi wa Misri, baada ya kurejea mahusiano mazuri baina ya nchi hizo mbili.

Ziara ya Al Sisi, Uturuki inafanyika kufuatia ziara iliyofanywa na Erdogan mjini Cairo mwezi Februari, ambayo ilikuwa ya kwanza tangu mwaka 2012 na ambayo ilifunguwa hatua kubwa ya kujengwa upya mahusiano yaliyokuwa yameharibika kwa muongo mzima.

Soma pia: Rais El Sissi azuru Uturuki baada ya kumaliza ya muongo mmoja madarakani

Viongozi hao wawili watajadili kuhusu mahusiano ya nchi hizo lakini pia watashauriana juu ya masuala kadhaa yanayoendelea kwa sasa kikanda na kimataifa na hasa kuhusu mashambulizi ya Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza na maeneo mengine ya ardhi ya Wapalestina.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW