1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJamhuri ya Moldova

Rais wa Moldova: Urusi ilipanga njama ya kuuangusha uongozi

13 Februari 2023

Rais wa Moldova Maia Sandu ameishutumu Urusi kuwa inapanga kutumia wahujumu wa kigeni kuuangusha uongozi wa taifa hilo dogo.

Berlin | Bundeskanzler Olaf Scholz empfängt moldauische Staatspräsidentin Maia Sandu
Picha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Sandu amesema hatua hiyo ya Urusi inalenga kuizuia nchi yake isijiunga na Umoja wa Ulaya na kutumia taifa hilo dogo katika vita vyake dhidi ya Ukraine.

Kulingana na Sandu, mpango unawahusisha raia wa Urusi, wa Montenegro, Belarus na Serbia na kuwawezesha kuingia Moldova kujaribu kuchochea maandamano katika jaribio la kubadilisha serikali rasmi na serikali haramu inayodhibitiwa na shirikisho la Urusi.

Sandu ametoa madai hayo baada yar ais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kusema wiki iliyopita kuwa nchi yake imegundua mpango wa kijaasussi wa Urusi wa kutaka kusababisha vurugu  Moldova.

Mara kadhaa, Sandu ambaye nchi yake inapakana na Ukraine ameelezea wasiwasi wake kuhusu nia ya Urusi kuelekea jamhuri hiyo ya iliyokuwa chini ya Umoja wa kisoviet kuhusiana na uwepo wa vikosi vya Urusi katika jimbo lililojitenga la Transdniestria.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW