1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Poland aikosoa Ulaya kwa kufungia fedha zake

21 Januari 2024

Rais wa Poland Andrzej Duda ameikosoa Halmashauri ya Ulaya kwa kuzuia fedha za mfuko wa Umoja wa Ulaya, kwa kile alichosema lilikuwa jaribio la kuilazimisha poland kuibadilisha serikali yake

Poland
Rais wa Poland Andrzej Duda Picha: Czarek Sokolowski/dpa/picture alliance

Serikali ya zamani ya Poland iliyoongozwa na chama cha kizalendo cha sheria na haki (PiS) ilihusika katika mvutano na Umoja wa Ulaya juu ya mageuzi ya mahakama na mfumo wa sheria hali iliyosababisha mabilioni ya fedha za Poland kuzuiliwa na Umoja huo. 

Donald Tusk aapishwa kuwa Waziri Mkuu mpya wa Poland

Serikali mpya inayounga mkono Umoja wa Ulaya, imeahidi kupata nafasi ya kufikia tena fedha hizo kwa kurejesha utawala wa sheria lakini inakabiliwa na changamoto kutoka kwa wafuasi na washirika wa chama cha serikali ya  akiwemo Duda na majaji wengine mashuhuri. 

Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya haikupatikana kutoa maoni juu ya taarifa hii. 
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW