1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Senegal akutana na baraza la mawaziri

Sylvia Mwehozi
15 Februari 2024

Rais wa Senegal Macky Sall amekutana na baraza lake la mawaziri jana, wakati akizidi kukabiliwa na shinikizo la ndani na kimataifa la kurejea katika kalenda ya uchaguzi.

Macky Sall
Rais wa Senegal Macky SallPicha: RTS/Reuters

Rais wa Senegal Macky Sall amekutana na baraza lake la mawaziri jana, wakati akizidi kukabiliwa na shinikizo la ndani na kimataifa la kurejea katika kalenda ya uchaguzi uliocheleweshwa na kutatua mzozo mkubwa wa kisiasa.Umoja wa Ulaya waitaka Senegal kutoa hakikisho la uhuru wa kimsingi

Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano wa rais na baraza lake la mawaziri, ilizungumzia kidogo juu ya mzozo wa kisiasa unaoendelea. Ofisi ya rais, imechapisha video kwenye mitandao ya kijamii ikihimiza mazungumzo ya wazi ya kitaifa kabla ya uchaguzi.

Marekani, Ufaransa na Umoja wa Mataifa zimeunga mkono matakwa ya Wasenegali ya kutaka upigaji kura ufanyike haraka iwezekanavyo.

Kumekuwa na hofu kwamba mvutano huo unaweza kuenea na kusababisha ghasia zaidi. Watu watatu wameuawa katika maandamano, tangu Rais Sall alipotangaza kuchelewesha uchaguzi hadi Desemba.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW