1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaLebanon

Rais wa Ujerumani aahidi kuendelea kuisaidia Lebanon

16 Februari 2026

Rais wa shirikisho la Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ameahidi kusadia juhudi za kurejesha utulivu nchini Lebanon, katika siku ya kwanza ya ziara ya siku mbili kwenye taifa hilo la Mashariki ya Kati.

Lebanon Beirut 2026 | Spika wa bunge la Lebanon Nabih Berri akimpokea Rais wa Shirikisho Frank-Walter Steinmeier
Rais wa Ujerumani Frank Walter Steinmeier(kulia) ameahidi akiwa ziarani nchini Lebabon kwamba ataendelea kulisaidia taifa hilo kurejesha utulivuPicha: Ibrahim Amro/AFP/Getty Images

Steinmeier amesema kwenye mkutano na waandishi wa habari sambamba na Rais wa Lebanon, Joseph Aoun kwamba Ujerumani itaendelea kushirikiana bega kwa bega na Lebanon.

Aidha ametoa wito kwa Lebanon na Israel kutimiza wajibu wao chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano ya mwaka 2025 ambayo aliyaelezea kama fursa kwa mataifa hayo yote mawili.

Makubaliano hayo kati ya Israel na Hezbollah yalifikiwa baada ya mapigano makali yaliyosababisha vifo vya watu 4,000 nchini Lebanon na 130 waliuawa Israel.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW