SiasaBrazil
Rais wa zamani wa Brazil agunduliwa na saratani ya ngozi
18 Septemba 2025
Matangazo
Hayo yameelezwa na daktari wake Claudio Birolini aliyewaambia waandishi wa habari kwamba Bolsonaro alipelekwa hospitalini kutokana na matatizo ya kutapika, kizunguzungu na shinikizo la damu.
Matatizo hayo ya kiafya yanajiri baada ya mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 70 kuhukumiwa wiki iliyopita kifungo cha miaka 27 jela kwa kosa la kupanga njama ya mapinduzi.
Wanasheria wa Bolsonaro wanatarajiwa kutumia hali hii ya kiafya kama kigezo cha kufanya maombi ya mteja wao kupewa kifungo cha nyumbani badala ya kulazimika kukaa gerezani.