1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa zamani wa Juan Orlando Hernandez Honduras

16 Februari 2022

Rais wa zamani wa Honduras Juan Hernandez amekamatwa na polisi nyumbani kwake kufuatia ombi la Marekani la kutaka kiongozi huyo apelekwe nchini humo kwa makosa yanayohusiana na biashara ya dawa za kulevya na silaha.

Honduras Korruption
Picha: Elmer Martinez/AP/picture alliance

Kukamatwa kwake kumetokea chini ya wiki tatu baada ya Hernandez kuachia madaraka na madai ya miaka kadhaa ya waendesha mashitaka wa Marekani yanayomuhusisha na walanguzi wa dawa za kulevya.

Hapo jana, jaji wa mahakama ya juu ya haki nchini Honduras aliyeteuliwa kushughulikia kesi yake, alisaini kibali cha kukamatwa kwa rais huyo wa zamani Juan Orlando Hernandez.

Hernandez anatuhumiwa kula njama na makundi ya kusafirisha dawa za kulevya na ufisadi katika taasisi nyingi za umma, kuzorota kwa shughuli za kijamii na kudhoofisha matumizi ya haki nchini Honduras.

Chanzo: reuters

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW