1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nicolas Sarkozy arudi tena mahakamani

7 Aprili 2026

Sarkozy atuhumiwa kuhusika na mpango wa kujipatia fedha kutoka serikali ya aliyekuwa rais wa Libya Muammar Gadhafi kwa ahadi ya kumuunga mkono kisiasa na kidioplomasia mnamo mwaka 2007.

Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy
Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy Picha: Julien De Rosa/AFP/Getty Images

Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy amerudishwa tena mahakamani leo Jumanne, kusikiliza kesi inayomuandama kuhusiana na tuhuma kwamba kampeini yake ya uchaguzi mwaka 2007 ilifadhiliwa kwa njia haramu kwa fedha kutoka Libya.

Kiongozi huyo wa zamani wa Ufaransa alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika na mpango wa kujipatia fedha kutoka serikali ya aliyekuwa rais wa Libya Muammar Gadhafi  kwa ahadi ya kumuunga mkono kisiasa na kidioplomasia.

Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy kwenda jela Jumanne

Hata hivyo mahakama ya rufaa mjini Paris baadae iliagiza aachiwe huru kusubiri kesi hii mpya ya rufaa,ambayo imepangwa kuendelea hadi mwezi Juni.

Kesi hiyo inatarajiwa kupitia upya ushahidi wote uliowasilishwa, unaohusiana na Sarkozy pamoja na washtakiwa wenzake 9 wakiwemo watatu waliokuwa mawaziri.

Sarkozy amekanusha mashtaka yanayomuandama akidai yalichochewa kisiasa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW