1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Rais Xi wa China awasili Cambodia kwa ziara ya siku mbili

17 Aprili 2025

Rais wa China Xi Jinping amewasili Alhamisi nchini Cambodia kwa ziara ya siku mbili ambayo inazingatiwa kama fursa ya kuimarisha mahusiano kati ya mataifa hayo mawili.

Phnom Penh 2025 | Rais wa China Xi Jinping akiwasili Cambodia
Rais wa China Xi Jinping akiwasili Cambodia kwa ziara ya siku mbiliPicha: STR/AFP/Getty Images

Xi atakutana na viongozi mbalimbali wa Cambodia ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu Hun Manet aliyesema hivi majuzi kuwa China ni mshirika muhimu ambaye ameisaidia nchi hiyo kiuchumi na kijamii.

Ziara hiyo ambayo ni ya kwanza tangu mwaka 2016, itahitimisha safari ya Xi kwenye nchi tatu za  kusini-mashariki mwa Asia  iliyozijumuisha Vietnam na Malaysia.

Katika miaka ya hivi karibuni, China imekuwa ikiongeza ushawishi wake katika eneo hilo kwa kutumia uwezo wake mkubwa wa kiuchumi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW