1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rajoelina amteua Waziri Mkuu mpya mwanajeshi

7 Oktoba 2025

Rais wa Madagascar Andry Rajoelina alimteua Jenerali Ruphin Fortunat Dimbisoa Zafisambo kuwa Waziri Mkuu, akitumaini kutuliza maandamano yanayoendelea dhidi ya uongozi wake ambayo yameitumbukiza nchi katika mgogoro.

Ufaransa Nice 2025 | Andry Rajoelina kabla ya chakula cha jioni cha Mkutano wa Bahari wa Umoja wa Mataifa
Rais wa Nice Madagascar Andry Rajoelina akiwa katika mji wa Riviera wa Ufaransa wa Nice, Juni 8, 2025.Picha: Patrick Aventurier/ABACAPRESS/IMAGO

Akizungumza akiwa ikulu, Rajoelina alisema waziri Mkuu mpya anapaswa "kuwahudumia wananchi" na awe "mtu safi, mwenye uadilifu, na anayefanya kazi kwa haraka." Pamoja na kiongozi huyo kutoa ahadi ya  kile alichokiita "tayari kuiokoa Madagascar", hatua yake ya kuvunja serikali nzima wiki iliyopita haikuweza kukidhi kiu ya waandamanaji.Maandamano hayo, ambayo yalianza kutokana na hasira dhidi ya kukatika kwa maji na umeme mara kwa mara katika kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi chenye umasikini, yamegeuka kuwa harakati za kupinga serikali zinazomtaka Rajoelina ajiuzulu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW