1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Robert Mueller: aliyeiongoza FBI Marekani afariki dunia

22 Machi 2026

Mkurugenzi wa zamani wa shirika la ujasusi la Marekani FBI Robert Mueller, aliyeongoza uchunguzi wa kisiasa kuhusu kampeni ya uchaguzi wa urais ya Donald Trump, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 81.

USA | Robert Mueller
Robert Mueller: aliyeiongoza FBI Marekani afariki wakiwa na umri wa miaka 81Picha: Photo12/picture alliance

Kifo chake kimesherehekewa hadharani na rais Trump.

Vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti vikinukuu taarifa ya familia ya Mueller kwamba mkurugenzi huyo wa zamani aliaga dunia Ijumaa jioni bila ya kutoa sehemu alipofia wala sababu ya kifo chake.

Baada ya tangazo hilo, rais Donald Trump aliandika katika mtandao wake wa Truth Social kwamba na hapa namnukuu " Robert Mueller amefariki, vizuri, nafurahi amekufa, na kwamba hawezi kuwaumiza tena watu wasiokuwa na hatia!" mwisho wa nukuu.

Licha ya kauli yake hiyo marais wengine wa zamani walijibu taarifa ya kifo cha Muller kwa kumtaja vizuri.

Barack Obama alimsifia Mueller akisema ni mfanyakazi aliyeheshimika kutokana na kazi yake huku George W. Bush, akisema amesikitishwa na kifo cha mueller aliyejitolea kuitumikia Marekani kwa nguvu zake zote.

 

    

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW