1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

RSF: Ghasia dhidi ya waandishi Kongo zinaongezeka

26 Machi 2026

Shirika la Waandishi habari wasiokuwa na mipaka RSF limesema leo kuwa waandishi wa habari wamekabiliwa na ongezeko la ghasia na shinikizo huku kukiwa na mzozo unaoongezeka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

 Berlin DW Afrika
Waandishi habari wa DW wakimhoji mkazi wa Berlin Picha: DW

RSF imesema waandishi wote wa mashariki mwa Kongo iliowahoji, wameripoti kwamba tangu kukamatwa kwa Goma mnamo Januari 2025, mbinu zao za kufanya kazi zimebadilika kabisa.

Imeongeza kuwa takriban waandishi wanane wamezuiwa na kundi la waasi la M23 ama huduma za kijasusi za jeshi la kawaida kwa siku kadhaa.

Kulingana na ripoti iliyochapishwa siku ya Jumanne, RSF imesema waandishi wawili walifungiwa na M23 kwenye makonteina yaliogeuzwa kuwa jela ambapo hadi wafungwa 80 walifungiwa kwa pamoja.

Ripoti hiyo pia imesema M23 iliwapa takriban waandishi wanne mafunzo ya kiitikadi, kudhibiti vipindi kwenye vituo vya redio vya ndani, na kulazimishia vipindi fulani au hoja za kuzungumzia

Wakati huo huo, ripoti hiyo imesema serikali imewashtumu waandishi wa habari kwa kuegemea upande wa M23 na washirika wake wa Rwanda.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW