1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio kukutana na Netanyahu Februari 28

19 Februari 2026

Afisa mmoja wa Marekani amesema kuwa waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Marco Rubio atasafiri na kuelekea Israel wiki ijayo wakati ambapo mivutano inazidi kati yake na Iran.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco RubioPicha: Bernadett Szabo/REUTERS

Afisa huyo ambaye hakutaka kutajwa jina amesema Rubio ataelekea Israel Februari 28 kukutana na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.

Netanyahu ambaye alifanya ziara Washington wiki iliyopita kwa mazungumzo na Rais Donald Trump, kwa muda amekuwa akitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Iran na Juni mwaka jana aliamrisha kampeni kubwa ya kuishambulia Tehran kwa mabomu.

Trump aliishia kujiunga na kampeni hiyo ambapo aliamrisha kushambuliwa kwa vinu vya nyuklia vya Iran.

Mnamo juzi Jumanne, Trump aliwatuma wajumbe wake kukutana na waziri wa mambo ya kigeni wa Iran, Abbas Arraghchi huko Geneva, Uswisi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW