1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rushdie apokea Tuzo ya Amani ya maonesho ya vitabu Ujerumani

23 Oktoba 2023

Rushdie amesema licha ya kupokea tuzo hiyo, amani ni dnto katika wakati ambapo uhuru unakandamizwa kote ulimwenguni.

Deutschland | Friedenspreis des Deutschen Buchhandels | Salman Rushdie
Salman Rushdie akipokea tuzo ya amani ya vitabu ya Ujerumani mjini Frankfurt, Oktoba 22.2023Picha: Kai Pfaffenbach/AP Photo/picture alliance

Mwandishi vitabu raia wa Uingereza mzaliwa wa India Salman Rushdie ametunukiwa tuzo ya amani ya maonyesho ya vitabu ya Ujerumani mjini Frankfurtjana Jumapili katika hafla iliyogubikwa na mizozo ya sasa duniani. Akizungumza katika kanisa la kihistoia mjini Frankfurt, Rushdie, mwenye umri wa miaka 76, alisema ameshukuru sana kwa tuzo hii kubwa lakini amani kwa sasa ni kama ndoto.

Rushdie aidha alisema tunaishi wakati ambao hakufikiri angeishi kuuona katika maisha yake ambapo uhuru, hususan wa kujieleza ambao bila huo ulimwengu wa vitabu haungekuwepo, unashambuliwa kote na kauli za misimamo mikali, kiimla, kizalendo na zisizojali.

Tuzo ya amani ya maonyesho ya vitabu ya Ujerumani inatolewa pamoja na kitita cha euro 25,000 na inachukuliwa kuwa tuzo muhimu zaidi nchini Ujerumani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW