1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rutte kuanza uongozi wa NATO

30 Septemba 2024

Waziri mkuu wa zamani wa Uholanzi, Mark Rutte, anatarajiwa kuchukua hatamu ya ukatibu mkuu wa Jumuiya ya Kijeshi ya NATO siku ya Jumanne (Oktoba 1).

NATO Mark Rutte
Waziri Mkuu wa zamani wa Uholanzi na mkuu mpya wa NATO, Mark Rutte.Picha: Robin van Lonkhuijsen/ANP/picture alliance

Katibu Mkuu anayemaliza muda wake, Jens Stoltenberg, ameliambia shirika la Habari la Reuters katika mahojiano siku ya Jumatatu (Septemba 30) kwamba nchi wanachama wa NATO hazipaswi kujizuia kutoa msaada zaidi wa kijeshi kwa Ukraine na kutokana na vitisho vya Rais Vladimir Putin wa Urusi anayesema anaweza kutumia silaha za nyuklia.

Soma zaidi: Putin asema Urusi itatimiza malengo yote yaliyowekwa Ukraine

Stoltenberg, atakabidhi uongozi wa Jumuiya ya NATO kwa Rutte baada ya kuhudumu kwa muongo mmoja.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW