1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda: Sherehe za Sikukuu ya walimu duniani

5 Oktoba 2009

<p>Serikali ya Rwanda imewaahidi waalimu kuwa italipatia ufumbuzi suala la mshahara mdogo ambalo limekuwa likiathiri ari yao katika utendaji kazi.

Kigali,mji mkuu wa Ruanda ambako kulikuwa na sherehe za Sikukuu ya walimuPicha: James Nzibavuga
Ahadi hiyo imetolewa na wizara ya elimu katika sherehe za kusherehekea siku kuu ya walimu duniani leo, katika sherehe mjini, Kigali. Katika sherehe hizo, walimu sitini walioongoza kwa ufanisi darasani walipewa tuzo zikiwemo kompyuta za laptop, pesa taslimu na vitabu. Juhudi hizi zinalenga kurejesha matumaini katika fani hii ya ualimu, ambao wengi wamekuwa wakiikimbia kwa kuwa haina maslahi kama fani nyingine.

Mwandishi wetu wa Kigali Daniel Gakuba ametuandalia taarifa ifuatayo.

Mwandishi: Daniel Gakuba

Mpitiaji Munira Muhammad

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW