Hatimaye Rwanda imevunja ukimya kuhusu moja ya mada zilizotawala mjadala wa usalama katika ukanda wa Maziwa Makuu kwa miaka mingi: uhusiano wake na kundi la waasi la AFC/M23. Kauli kutoka kwa Balozi wa Rwanda nchini Marekani, Mathilde Mukantabana, imeweka wazi kile ambacho kwa muda mrefu kimekuwa kikisemwa na wadau wa kimataifa, lakini Kigali imekanusha vikali.