Saif al-Islam Gaddafi auawa
4 Februari 2026
Kwa mujibu wa wakili wake, Khaled al-Zaidi, Saif aliuawa na watu wanne waliokuwa wameficha sura zao walioivamia ofisi yake siku ya Jumanne (Februari 3).
Kituo cha televisheni cha al-Arabiya, kimeripoti kwamba Saif, aliyekuwa na umri wa miaka 53, aliuawa akiwa kwenye bustani ya nyumba yake huko Zintan, kikimnukuu mtu wa karibu na familia ya Gaddafi.
Kulikuwa na uvumi kwamba wanamgambo walio karibu na serikali yenye makao yake mjini Tripoli inayoongozwa na Waziri Mkuu Abdul Hamid Dbeibeh wamehusika na mauaji hayo, ingawa wenyewe wamekanusha.
Saif al-Islam alikuwa anasemakana kupanga kurejea kwenye siasa, hatua iliyotazamwa kama kikwazo kwa Dbeibeh na washirika wake.
Hadi kifo chake, mtoto huyo wa Gaddafi alikuwa akitakiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kujibu mashitaka ya uhalifu dhidi ya ubinaadamu wakati wa machafuko ya Libya.