1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Saka aipeleka Arsenal fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

Josephat Charo
6 Mei 2026

Arsenal imefuzu kuingia fainali ya kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya Champions kwa mara ya pili katika historia yao katika kipindi cha miaka 20.

Bao la nahodha Bukayo Saka lilitosha kuwapa ushindi Artsenal dhidi ya Atletico Madrid.
Bao la nahodha Bukayo Saka lilitosha kuwapa ushindi Artsenal dhidi ya Atletico Madrid.Picha: Neal Simpson/Imago Images

Arsenal imefuzu kuingia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Champions kwa mara ya pili katika historia yao kwa ushindi wa nyumbani wa 1-0 dhidi ya Atletico Madrid na kuihakikishia ushindi wa jumla wa 2-1 katika nusu fainali jana Jumanne.

Bao la nahodha Bukayo Saka muda mfupi kabla kipindi cha kwanza kukamilika lilithibitisha kuwa muhimu kwa Arsenal kushinda pambano gumu ambapo wenyeji waliweka rekodi ya tisa ya kutofungwa katika mashindano ya msimu huu.

Arsenal watakabiliana na mabingwa watetezi Paris St Germain, ambao waliwatoa katika nusu fainali ya msimu uliopita, au Bayern Munich katika uwanja wa Puskas mjini Budapest mnamo Mei 30.

Fainali pekee ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa ilikuwa mwaka wa 2006 waliposhindwa na Barcelona.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW