Sala ya kwanza ya Ijumaa ya Ramadhani yafanyika Jerusalem
20 Februari 2026
Matangazo
Sala hiyo huko Al-Aqsa, yalifanyika kwa mara ya kwanza tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Hamas kuanza kutekelezwa mwezi Oktoba.
Ilikuwa fursa ya kwanza ambapo watu wengi waliondoka Ukingo wa Magharibi na kusali katika eneo hilo la mji mkongwe wa Jerusalem tangu kipindi cha Ramadhani mwaka jana.
Lakini Israel ilidhibiti idadi ya Wapalestina walioruhusiwa kuingia kutoka Ukingo wa Magharibi hadi 10,000 na iliruhusu tu kuingia kwa wanaume wenye umri wa zaidi ya miaka 55 na wanawake wa umri wa zaidi ya miaka 50 pamoja na watoto wa umri wa hadi miaka 12.
Awali iliweka vikwazo sawa na hivyo kutokana na wasiwasi wa kiusalama.