Samia Suluhu Hassan aapishwa rasmi kuwa rais wa Tanzania
3 Novemba 2025
Matangazo
Rais Samia ameingia madarakani kuongoza muhula wa pili baada ya kupewa ushindi wa asilimia 98 ya kura na Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania (INEC).
Hafla ya kuapishwa kwake imefanyika chini ya ulinzi mkali katika uwanja wa kijeshi mjini Dodoma.
Kiongozi huyo ameapishwa huku upinzani ukiyakataa matokeo yaliyommpa ushindi na kusema mchakato wa uchaguzi haukuwa wa huru na Haki.
Hali bado ni tete nchini humo kufuatia maandamano yaliyozuka muda mfupi baada ya uchaguzi kuanza.