1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Saudi Arabia yatangaza mkutano wa kuichangia Sudan

14 Juni 2023

Saudi Arabia imetangaza mkutano wa kimataifa wiki ijayo kukusanya ahadi za msaada kwa Sudan iliyoharibiwa kwa vita, ambapo Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya nusu ya idadi ya watu wanahitaji msaada na ulinzi haraka.

Saudi-Arabien Friedensverhandlungen zum Sudan in Dschidda
Picha: Saudi Press Agency/REUTERS

Likunukuu wizara ya mambo ya kigeni shirika rasmi la Saudi Arabia limesema mkutano huo wa ahadi utafanyika Juni 19, na kuongeza kuwa utaongozwa kwa pamoja na Qatar, Misri, Ujerumani na Umoja wa Ulaya, pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa takribani watu milioni 25 ikiwa ni zaidi ya idadi jumla ya watu wa taifa hilo wanauhitaji wa msaada na ulinzi, lakini  mwishoni mwa Mei kulitolewa dola milioni 2.6 katika kukabiliana na shida hiyo ikiwa sawa na asilimia 13 tu.

Soma pia: Marekani na Saudi Arabia zashtumu vikali kurejea kwa mapigano nchini Sudan baada ya kusitishwa kwa saa 24

Kwa zaidi ya majuma manane Saudi Arabia na Marekani zimekuwa katika juhudi za upatanishi kati ya mkuu wa jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan na makamu wake wa zamani Mohamed Hamdan Daglo ambaye anaongoza kikosi cha kijeshi cha dharura.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW