1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SAUDIA YAITETEA SYRIA

22 Februari 2005

RIYADH:

Waziri wa nje wa Saudi Arabia,mwanamfalme Saud al-Feisal amesema nchi zisifyatuke tu kuilaumu Syria kuhusika na mauaji ya waziri-mkuu wa zamani wa Lebanon, Rafik Hariri.

Waziri huyo wa Saudia alipinga pia mwioto wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa juu ya kifo cha Hariri.Alisema, Lebanon iachiwe ifanye uchunguzi wake binafsi.

Viongozi wa Upinzani nchini Lebanon wamekuwa wakiinyoshe kidole syria kuhusika na mauaji ya Bw.Hariri.

Marehemu alikua na usuhuba mkubwa na mfalme wa saudi Arabia na alikua na uraia pia wa Saudia mbali na ule wa Lebanon.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW