1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz ashiriki maadhimisho ya miaka 80 ya kumpinga Hitler

20 Julai 2024

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholzametoa wito kwa watu kuendelea kuitetea demokrasia na uhuru katika maadhimisho ya miaka 80 tangu lilipofanyika jaribio la kumuua kiongozi wa wanazi Adolf Hitler

Berlin | Olaf Scholz
Kansela wa Ujerumani Olaf Scholzametoa wito kwa watu kuendelea kuitetea demokrasia na uhuru katika maadhimisho ya miaka 80 tangu lilipofanyika jaribio la kumuua kiongozi wa wanazi Adolf HitlerPicha: Hannes P Albert/dpa/picture alliance

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz ametoa wito kwa watu kuendelea kuitetea demokrasia na uhuru katika maadhimisho ya miaka 80 tangu lilipofanyika jaribio la kumuua kiongozi wa wanazi Adolf Hitler.

Soma zaidi. Jeshi la Ujerumani lina utayari kubeba dhamana NATO?

Scholz amesisitiza kwa kusema kuwa Ujerumani bora ni ile inayofuata misingi ya katiba ya nchi yake na kwamba raia wa kawaida wa Ujerumani yenye demokrasia hawahitaji kufanya vitendo vya kutishia maisha yao kama vile maofisa wa jeshi walioongozwa na Claus Schenk von Stauffenberg, ambaye alijaribu kumuua Hitler kwa bomu bila mafanikio.

Kansela Olaf Scholz amesema demokrasia ya Ujerumani inategemea juhudi za kila mmoja bila kuchoka na kwamba watu wanapaswa kupinga kwa nguvu misimamo na mitazamo mikali.


 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW