1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz azirai EU na China kujadiliana mvutano kuhusu ushuru

24 Juni 2024

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amezihimiza China na Umoja wa Ulaya kutumia fursa ya mazungumzo yaliyoanzishwa ya kutatua mzozo kuhusu mapendekezo ya ushuru wa magari ya umeme yanayoagizwa kutoka China.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz
Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.Picha: Markus Schreiber/AP Photo/picture alliance

Akizungumza katika kongamano la kila mwaka la Shirikisho la Viwanda la Ujerumani, BDI na lenye ushawishi mkubwa, Scholz amesema ni "muhimu" kwa Umoja wa Ulaya na Beijing kufikia maelewano ifikapo mwisho wa mwezi.

Waziri wa Uchumi wa Ujerumani Robert Habeck, amesema kuna hatari ya kila upande kupoteza kunapokuwa na vita vya biashara vinavyosababishwa na ongezeko la ushuru, baada ya wiki iliyopita kusisitizia umuhimu wa mazungumzo, alipozuru China.

Umoja wa Ulaya ulipanga kupandisha ushuru kutoka asilimia 17.4 hadi 38.1 wa magari hayo kwa muda wa miezi minne, kuanzia Julai 4, hatua iliyochochea mzozo wa kibiashara.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW