1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSenegal

Senegal: Upinzani washtumu mamlaka juu ya tarehe ya uchaguzi

21 Februari 2024

Wagombea wa kambi ya upinzani katika uchaguzi wa urais nchini Senegal wamezishutumu mamlaka kwa kujiburuza kuchukua hatua ya kupanga tarehe mpya ya uchaguzi.

Senegal Dakar | Khalifa Sall, kiongozi wa vuguvugu la Taxawu
Khalifa Sall, kiongozi wa vuguvugu la Taxawu ambaye pia ni mgombea wa urais nchini SenegalPicha: Seyllou/AFP/Getty Images

Hii ni baada ya mahakama kupitisha uamuzi uliobatilisha hatua ya kuuchelewesha kwa miezi 10 uchaguzi huo.

Rais wa nchi hiyo Macky Sall wiki iliyopita aliahidi kwamba atazingatia ombi lililotolewa na baraza la katiba la kutaka uchaguzi huo upangwe haraka iwezekanavyo. 

Mahakama iliitupilia mbali amri ya Rais Macky Sall iliyoungwa mkono na bunge iliyouakhirisha uchaguzi huo uliopangwa awali kufanyika tarehe 25 mwezi huu wa Februari.

Hata hivyo bado tarehe mpya mpaka sasa haijatangazwa hali ambayo imeibuwa wasiwasi miongoni mwa wagombea wa upinzani ambao baadhi wanashinikiza uchaguzi ufanyike kabla ya muhula wa pili wa Rais Macky Sall haujamalizika tarehe 2 mwezi Aprili.

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW