1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Seneti imepinga mswada wa deni Marekani

30 Julai 2011

Baraza la seneti linalodhibitiwa na chama cha Democratic nchini Marekani liliupinga mswada wa kupandisha kiwango cha ukopaji wa serikali kupitia kura 59 dhidi ya 41

Rais Barack Obama wa MarekaniPicha: dapd

Hii ni baada ya baraza la wawakilishi nchini Marekani limeidhinisha pendekezo la chama cha Republican, kupandisha kiwango cha ukopaji cha nchi hiyo katika awamu mbili, kupitia kura 218 dhidi ya 210.

Majadiliano ya suala zitoPicha: picture alliance/dpa

Baadhi ya wanachama wa Republican walijiunga na wale wa Democratic kupinga hatua hiyo ya wabunge wenzao.

Wasiwasi ulizidi kufuatia kuwadia siku ya Ijumanne ambayo wizara ya fedha ya Marekani inasema ndio siku ya mwisho kuwa na akiba ya kutosha ili kuweza kutekeleza wajibu wake wa kuwalipa wamiliki wa hisa za serikali pamoja na wastaafu, maskini, na wale wanaohitaji huduma za afya.

Spika wa bunge John BoehnerPicha: AP

Spika wa bunge John Boehner aliahirisha kura hiyo kwa siku mbili, akibishana na wanachama wenzake katika jitahada ya kuwashawishi kuunga mkono mpango huo.

Mwandishi: Maryam, Abdalla/Dpae/Rtre
Mhariri:Martin, Prema

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW