1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiMarekani

Serikali kutoa msaada baada ya vimbunga huko Mississipi

26 Machi 2023

Rais wa Marekani Joe Biden ametoa tamko la dharura hii leo kufuatia vimbunga vilivyoshuhudiwa tangu siku ya Ijumaa katika Jimbo la kusini mwa Marekani la Mississippi na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 26.

USA | Schäden nach Tornado in Mississippi
Picha: Lokman Vural Elibol/AA/picture alliance

Biden amesema msaada wa serikali ya shirikisho utapelekwa katika maeneo yaliyoathirika. Hali mbaya zaidi ya hewa ikiambatana na mvua kubwa na upepo mkali inatarajiwa tena hii leo huko Mississippi.

Shirika la usimamizi wa dharura la serikali limeonya kwamba huenda kukashuhudiwa pia vimbunga. Vikosi vya uokoaji bado vinaendelea kuwasaka manusura.

Soma pia: Vimbunga vyasababisha vifo vya watu 26 huko Mississippi, Marekani

Baadhi ya vitongoji vimeathirika pakubwa ikiwemo kile cha Rolling Fork chenye wakazi takriban 2000, ambako majengo yote yameharibika. Vimbunga huripotiwa mara kwa mara nchini Marekani hasa katika maeneo ya kati na kusini mwa nchi hiyo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW