1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guinea yavifuta vyama 40 vya siasa

7 Machi 2026

Serikali ya Guinea imevifuta vyama 40 vya kisiasa vikiwemo vyama vikubwa vya upinzani. Amri ya kuvifuta vyama hivyo imetangazwa na Wizara ya Utawala kwa madai kuwa vyama hivyo vimeshindwa kutimiza majukumu yao.

Guinea imevifuta vyama 40 vya siasa
Rais wa Guinea Mamady DoumbouyaPicha: Issouf Sanogo/AFP/Getty Images

Kulingana na agizo hilo vyama vilivyopigwa marufuku havitambuliki tena kisheria na vinapaswa kusimamisha shughuli zote mara moja. Vyama hivyo vimepigwa marufuku kutumia nembo zao, majina au alama, na mali zao zitataifishwa na kudhibitiwa na serikali.

Karibu miezi miwili baada ya Doumbuya kuingia mamlakani

Hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni chini ya miezi miwili tangu kiongozi wa kijeshi Mamady Doumbouya alipoapishwa kuwa rais wa Guinea. Asasi za kiraia zimeukosoa uamuzi huo ziliouita wa kidikteta.

Vyama vilivyofutwa ni pamoja na UFDG kilichokuwa chini ya uongozi wa Cellou Dalein Diallo aliye uhamishoni, RPG  cha Rais wa zamani Alpha Conde, na chama cha UFR.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW