1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali ya Kongo na M23 zasaini makubaliano ya amani

15 Novemba 2025

Wawakilishi wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wale wa kundi la waasi la M23 wametia saini leo Jumamosi nchini Qatar, makubaliano ya mpango wa amani unaolenga kukomesha mapigano mashariki mwa Kongo.

Qatar Doha 2025 | makubaliano ya mpango wa amani wa serikali ya Kongo na M23
Mwakilishi wa serikali ya Kongo Sumbu Sita Mambu( kushoto) na katibu mtendaji wa kundi la M23 linaloungwa mkono na Rwanda Benjamin Mbonimpa (kulia) baada ya kusaini makubaliano ya amani mjini Doha mnamo Julai 19, 2025Picha: Karim Jaafar/AFP

Kuanzia mwezi Aprili mwaka huu, Qatar iliandaa na kusimamia raundi kadhaa za mazungumzo ya moja kwa moja kati ya serikali ya Kongo na waasi hao wa M23 na tangu wakati huo kumekuwa kukijadiliwa masharti ya awali pamoja na kujenga mazingira ya pande hizo hasimu kuaminiana.

Pande hizo mbili zilisaini mwezi Julai tamko la kanuni ambalo halikuweka wazi namna ya kushughulikia masuala mengi muhimu ambayo ndiyo chanzo cha mzozo huo, na mwezi Oktoba hatimaye mahasimu hao walifikia makubaliano kuhusu hatua za ufuatiliaji wa kusitisha mapigano.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW