1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waasi wa ADF washutumiwa kwa kushambulia migodi na kuua raia

16 Machi 2026

Serikali nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema kundi la waasi na la Allied Democratic Forces, ADF lilishambulia migodi iliyoko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo na kusababisha vifo vya raia.

DR Kongo | Luhihi-Mgodi wa dhahabu katika mkoa wa mashariki wa Kivu Kusini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yalishutumu kundi la waasi wa ADF kwa kushambulia migodi na kuua raiaPicha: Alexis Huguet/AFP/Getty Images

Taarifa hii ya jana Jumapili ya serikali imesema ADF linalodai kuwa na mafungamano na kundi linalojiita Dola la Kiislamu, IS, Jumatano iliyopita lilivamia migodi ya dhahabu iliyo karibu na mikoa ya Muchacha na Ituri.

Kulingana na serikali, shambulizi hilo ambalo IS ilidai kulifanya lilisababisha vifo vya raia baadhi ya majengo kuungua na wakazi wengi kuyakimbia makazi yao.

Kundi la ADF lililoanzishwa na waasi wa nchini Uganda limekuwa likishutumiwa kwa mauaji ya halaiki na uporaji huko Ituri na jimbo jirani la Kivu Kaskazini, katikati ya machafuko yaliyogubika mashariki mwa Kongo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW