Miaka 10 Jela kwa Sheikh Hasina kwa makosa ya ufisadi
2 Februari 2026
Mpwa wa Sheikh Hasina Tulip Siddiq ambaye ni mbunge nchini Uingereza alihuhukumiwa pia kifungo cha miaka 4 jela, katika kesi mbili walizokabiliwa nazo zinazohusiana na Ufisadi.
Jaji Mohammed Rabiul Alam pia alitoa hukumu nyengine ya miaka 7 kwa watu wengine wawili wa familia ya Sheikh Hasina, Azmina Siddiq an Radwan Mujib Siddiq kwa makosa sawa na hayo.
Taasisi ya kupambana na rushwa ya Bangladesh ilianzisha kesi mahakamani dhidi ya waziri Mkuu huyo wa zamani, ikidai alishirikiana na maafisa wa serikali ili kujipatia yeye na familia yake ploti sita katika mpango wa serikali wa Purbachal karibu na mji mkuu Dhaka licha ya kanuni za serikali kumbana kufanya hivyo.
Uamuzi huo umetokea wakati serikali ya mpito inayoongozwa na aliyewahi kushinda Tuzo ya amani ya Nobel Muhammad Yunus, ikijitayarisha kwa uchaguzi unaoatarajiwa kufanyika Februari 12. Chama cha Hasina cha zamani cha Awami kimepigwa marufuku kushiriki.