1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUingereza

Sheria mpya dhidi ya migomo yaanza kutumika Uingereza

2 Julai 2023

Sheria mpya inayowapa polisi mamlaka zaidi katika kuchukua hatua dhidi ya migomo imeanza kutumia rasmi leo Uingereza. Sheria hiyo inawalenga hasa wanaharakati wanaovuruga shughuli kwa kufanya maandamano.

Frankreich, Nizza | Proteste und Ausschreitungen nach dem Tod eines 17-jährigen
Picha: /Cyril Dodergny/NICE MATIN/PHOTOPQR/MAXPPP/dpa/picture alliance

Chini ya sheria hiyo mpya, polisi sasa inaweza kuwahamishia mahali pengine waandamanaji wanaosababisha usumbufu kwa vyombo vya usafiri. Katika sheria hiyo pia, waandamanaji watakaopatikana na hatia ya kuzuwia ujenzi wa miundombinu mipya wanaweza kukabiliwa na hukumu ya kifungo cha miaka mitatu jela.

Maandamano ya wanamazingira yamekuwa yakilaaniwa

Pamoja na hayo, mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kuzuia mradi mkubwa wa usafiri anaweza kufungwa jela kwa kipindi cha miezi sita. Mamlaka nchini humo mara kwa mara zimekuwa zikiyalaani maandamano ya wanamazingira wakiwemo wa makundi ya "Just stop oil na "Extinction Rebellion" ambao wanahamasishaji juu ya dharura ya mabadiliko ya tabia nchi kwa kufanya maandamano makubwa kwenye barabara zenye magari mengi. Hata hivyo, wakosoaji wanasema sheria kali ni kitisho kwa haki ya kuandamana .

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW