1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shirika la kutetea haki Tunisia lafungiwa kufanya kazi zake

25 Aprili 2026

Serikali ya Tunisia imeliamuru Shirika la Tunisia la Kutetea Haki za Binadamu, LTDH, lililowahi kuwa mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel ya mwaka 2015 kusimamisha shughuli zake kwa mwezi mmoja.

Shirika la kutetea haki za binadamu la Tunisia LTDH limefungiwa kufanya shughuli zake kwa mwezi mmoja
Wanachama wa Shirika la Kutetea Haki za Binadamu Tunisia kwenye maandamano ya kuadhimisha miaka 77 ya Azimio la Haki za BinadamuPicha: Chedly Ben Ibrahim/NurPhoto/picture alliance

Rais wa shirika hilo Bassem Trifi, amesema uamuzi huo umetolewa na mahakama ya mwanzo ya Tunisia na kwamba watakata rufaa. LTDH imeutaja uamuzi huo kuwa wa hatari, usiofuata haki wala misingi iliyo wazi.

Serikali yataja dosari za kiutawala

Shirika hilo limeelezwa kuwa shughuli zake zimesimamishwa kutokana na dosari za kiutawala, madai ambayo yameshawahi kutumika dhidi ya mashirika mengine yasiyo ya kiserikali. Tangu mwaka jana, zaidi ya mashirika 17 yamesimamishwa kwa muda nchini humo. Mashirika yakutetea haki za binadamu yamekuwa yakiikosoa serikali ya Rais Kais Saied kwa kukandamiza uhuru wa kiraia nchini humo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW