Shughuli ya mavuno inayoambatana na burudani Jamii ya kabila la Wasukuma lilinalopatikana katia mikoa ya Kanda ya Ziwa nchini Tanzania, hualikana katika shughuli za kilimo na uvunaji ili kurahisisha kazi. Wakati wa mavuno Wasukuma hutumia njia ya kuimba na kucheza, huku mwenye shamba akiandaa chakula kwa ajili ya marafiki wanaokwenda kumsaidia shughuli za shambani.