1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SINGAPORE: Ujerumani yapinga kiti kimoja kwa eneo la Euro

16 Septemba 2006

Waziri wa fedha wa Ujerumani,Peer Steinbrück amepinga mashauri yaliyopendekezwa kuwa mataifa 12 yanayotumia sarafu ya Euro yawe na kiti kimoja katika bodi ya Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF.Mapendekezo hayo yametolewa kama sehemu ya mageuzi mbali mbali yanayofanywa katika taasisi hiyo.Waziri Steinbrück anaehudhuria mikutano ya mwaka ya IMF na Benki Kuu ya Dunia nchini Singapore amesema,Ujerumani ikishika nafasi ya tatu kiuchumi duniani,baada ya Marekani na Japan,lazima iendelee kuwa na usemi katika IMF. Hivi sasa shirika hilo linatafuta njia ya kuzipa nchi zinazonyanyuka kiuchumi,kama vile China, usemi zaidi katika uongozi wa taasisi hiyo yenye wanachama 184 na ambayo hutoa mikopo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW