1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Soka. Bayern yaonja kipigo.

11 Novemba 2007

Katika ligi ya soka ya Ujerumani mabingwa watetezi VFB Stuttgart wamewashindwa Bayern Munich kwa jumla ya mabao 3-1. Hiki ni kipigo cha kwanza kwa Bayern katika msimu huu wa Bundesliga, lakini wamebaki wakiongoza ligi hiyo licha ya kipigo hicho . Katika michezo mingine ya Bundesliga Rostock iliishinda Energy Cottbus kwa mabao 3-2, Hertha BSC Berlin ikaishinda Hanover kwa bao 1-0, Werder Bremen ikaizamisha Karlsruhe kwa mabao 4-0, Schalke 04 ikatoka sare ya bao 1-1 na Hamburg SV na Borussia Dortmund nayo ikatoka sare pia ya bao 1-1 na Eintracht Frankfurt.