1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Soko la sukari la Umoja wa Ulaya kurekebishwa

25 Novemba 2005

Mawaziri wa kilimo wa UU waafikiana kurekebisha soko lao la sukari .Hivyo waitikia shinikizo klutoka Shirika la Biashara Duniani (WTO).Programm: Afrikanische Sprachen - Kiswahili Manuskript Nr. Kostenstelle 9426 Tag 25.11.2005 Lfd. Nr. 1 Pos. Nr. 86 EDV-Nr.: 623884 21 Manuskripttitel: EU Zuckermarkt Kurztitel Programmtitel/Sendung: Journal I * Autor: Ulrike Bosse ID. Nr. In diesem Ms wurden geschützte Beiträge anderer Urheber verwendet. Ggfs. ankreuzen und genaue Angaben dem Ms beifügen. Ja * * Bearbeiter: Ramadhan Ali ID. Nr. 10 23 65 * Übersetzer: ID. Nr. Redaktion: Programmart: Honoraranforderung für * * * Stufe DM - Betrag Mod. Baada ya majadiliano marefu mawaziri wa kilimo

wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana huko Brussels kufanya mageuzi makubwa kurekebisha utaratibu wa soko la sukari uliotumika miaka 40 sasa . Kwa maafikiano hayo ya kufanya marekebisho, viwanda vya sukari vya Ulaya na wakulima wa mimea inayotengezewa sukari, watapaswa kuridhia kupungukiwa na mapato.Kwani, shabaha ya marekebisho hayo, ni kuachana na mtindo wa kudhamini bei walizohakikishiwa hadi sasa wakulima na viwanda vya sukari barani Ulaya.Imepangwa pia kuwafidia kwa kadiri fulani wakulima na viwanda hivyo kwa kupungukiwa na mapato. Mageuzi haya katika Umoja wa Ulaya yalilazimika kwavile Shirika la Biashara duniani (WTO) likuangalia utaratibu uliotumiwa hadi sasa ni kukiuka kanuni za kimataifa za biashara.Beik za sukari ndani ya nchi za Umoja wa Ulaya hivi sasa ni kubwa mara tatu kuliko zilivyo katika soko la dunia.Uchambuzi wa ulrike Bosse kutoka Brussels, mnasimuliwa studioni na Ramadhan Ali: Umoja wa Ulaya na sera zake za kilimo mwishoe, waafikiana kuleta mageuzi.Na pale mwishoe, rais wa Jumuiya ya wakulima wa Ujerumani pamoja na waziri wa kilimo wa Ujerumani walipokaa pamoja katika meza ya kikao cha mwisho cha mkutano huu, ni ushahidi dhahiri kwamba, walioathrika na mageuzi hayo hawakuachwamkono kabisa. Ni wazi kwamba, wakulima wa matunda yanayotengezewa sukari huku Ulaya hawashangirii maafikiano yaliofikiwa Brussels,kwani fidia walipwazo zinapunguzwa na hii, ina maana mapato yao yanapungua.Lakini, wale wakulima ambao ni wa kweli miongoni mwao,wameungama binafsi katika mvutano wa kufanya mageuzi haya wiki chache zilizopita, kwamba wakineemeka mno kutokana na ukarimu wa Umoja wa Ulaya. Wakati katika sekta nyengine za kilimo mageuzi tayari yamepitishwa,hakujafanyika mabadiliko yoyote katika zao la sukari tangu kupita miaka 4o sasa.Laiti Shirika la Biashara Duniani halingetoa hukumu dhidi ya fidia walipwazo wakulima wa UU,basi majadiliano yangeeendelea ndani kwenyewe katika UU. Mabishano juu ya matumizi makubwa yanayokwenda katika mfuko wa kilimo ndani ya UU ni ushahidi wa hayo.Wazi kwamba mkulima huyu au yule wa kijerumani hamuelewi rais wa jumuiya ya wakulima wa Ujerumani Sonnleitner akisema kuwa, kilimo cha mimea inayotengezewa sukari nchini Ujerumani kimeokolewa kwavile anatoa sababu Ujerumani si mahala pema pa upandaji nafuu wa zao hilo wakati huu na kuna maeneo mengi ya kupandisha zao hilo nchini Ujerumani kwenyewe.Ni katika mashamba kama hayo anabashiri waziri mpya wa kilimo wa Ujerumani Bw.seehöfer,ulimaji utatuwama.Kwa wakulima wengine ambao watahisi kupandisha zao hili la sukari hakuna faida tena ,wataachana kabisa na upandaji.Na hili ni pigo kwa baadhi ya wakulima, lakini ndio hali halisi iliowakumba wafanyikazi wa viwandani. Kwa waziri mpya wa kilimo wa Ujerumani Bw.seehofer,yafaa kuongeza kusema ingawa majadiliano yalikua marefu mjini Brussels,hayakua mwanzo mbaya kwake kama waziri wa kilimo wa serikali mpya ya Ujerumani. Alipofunga safari kwenda Brussels,alisema kwamba anaungamkono mageuzi katika soko la zao la sukari lakini akitazamia marekbisho bora kutoka mashauri ya aywali ya mageuzi hayo katika sekta ya bei,katika msaada unaotolewa kulistawisha zao hilo na kuwalinda wakulima wasidhurike na uagizaji wa sukari usiodhibitiwa kutoka n’gambo. Yote hayo, waziri Seehofer amefanikiwa Brussels,kwavile hata wanachama wengine wa UU wakitaka vivyo hivyo.

Baada ya majadiliano marefu mawaziri wa kilimo wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana huko Brussels kufanya mageuzi makubwa kurekebisha utaratibu wa soko la sukari uliotumika miaka 40 sasa .

Kwa maafikiano hayo ya kufanya marekebisho, viwanda vya sukari vya Ulaya na wakulima wa mimea inayotengezewa sukari, watapaswa kuridhia kupungukiwa na mapato.Kwani, shabaha ya marekebisho hayo, ni kuachana na mtindo wa kudhamini bei walizohakikishiwa hadi sasa wakulima na viwanda vya sukari barani Ulaya.Imepangwa pia kuwafidia kwa kadiri fulani wakulima na viwanda hivyo kwa kupungukiwa na mapato.

Mageuzi haya katika Umoja wa Ulaya yalilazimika kwavile Shirika la Biashara duniani (WTO) likuangalia utaratibu uliotumiwa hadi sasa ni kukiuka kanuni za kimataifa za biashara.Beik za sukari ndani ya nchi za Umoja wa Ulaya hivi sasa ni kubwa mara tatu kuliko zilivyo katika soko la dunia.Uchambuzi wa ulrike Bosse kutoka Brussels, mnasimuliwa studioni na Ramadhan Ali:

Umoja wa Ulaya na sera zake za kilimo mwishoe, waafikiana kuleta mageuzi.Na pale mwishoe, rais wa Jumuiya ya wakulima wa Ujerumani pamoja na waziri wa kilimo wa Ujerumani walipokaa pamoja katika meza ya kikao cha mwisho cha mkutano huu, ni ushahidi dhahiri kwamba, walioathrika na mageuzi hayo hawakuachwamkono kabisa.

Ni wazi kwamba, wakulima wa matunda yanayotengezewa sukari huku Ulaya hawashangirii maafikiano yaliofikiwa Brussels,kwani fidia walipwazo zinapunguzwa na hii, ina maana mapato yao yanapungua.Lakini, wale wakulima ambao ni wa kweli miongoni mwao,wameungama binafsi katika mvutano wa kufanya mageuzi haya wiki chache zilizopita, kwamba wakineemeka mno kutokana na ukarimu wa Umoja wa Ulaya.

Wakati katika sekta nyengine za kilimo mageuzi tayari yamepitishwa,hakujafanyika mabadiliko yoyote katika zao la sukari tangu kupita miaka 4o sasa.Laiti Shirika la Biashara Duniani halingetoa hukumu dhidi ya fidia walipwazo wakulima wa UU,basi majadiliano yangeeendelea ndani kwenyewe katika UU.

Mabishano juu ya matumizi makubwa yanayokwenda katika mfuko wa kilimo ndani ya UU ni ushahidi wa hayo.Wazi kwamba mkulima huyu au yule wa kijerumani hamuelewi rais wa jumuiya ya wakulima wa Ujerumani Sonnleitner akisema kuwa, kilimo cha mimea inayotengezewa sukari nchini Ujerumani kimeokolewa kwavile anatoa sababu Ujerumani si mahala pema pa upandaji nafuu wa zao hilo wakati huu na kuna maeneo mengi ya kupandisha zao hilo nchini Ujerumani kwenyewe.Ni katika mashamba kama hayo anabashiri waziri mpya wa kilimo wa Ujerumani Bw.seehöfer,ulimaji utatuwama.Kwa wakulima wengine ambao watahisi kupandisha zao hili la sukari hakuna faida tena ,wataachana kabisa na upandaji.Na hili ni pigo kwa baadhi ya wakulima, lakini ndio hali halisi iliowakumba wafanyikazi wa viwandani.

Kwa waziri mpya wa kilimo wa Ujerumani Bw.seehofer,yafaa kuongeza kusema ingawa majadiliano yalikua marefu mjini Brussels,hayakua mwanzo mbaya kwake kama waziri wa kilimo wa serikali mpya ya Ujerumani.

Alipofunga safari kwenda Brussels,alisema kwamba anaungamkono mageuzi katika soko la zao la sukari lakini akitazamia marekbisho bora kutoka mashauri ya aywali ya mageuzi hayo katika sekta ya bei,katika msaada unaotolewa kulistawisha zao hilo na kuwalinda wakulima wasidhurike na uagizaji wa sukari usiodhibitiwa kutoka n’gambo. Yote hayo, waziri Seehofer amefanikiwa Brussels,kwavile hata wanachama wengine wa UU wakitaka vivyo hivyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW