1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSenegal

Sonko aigomea serikali mpya ya Faye

2 Juni 2026

Rais Bassirou Diomaye Faye wa Senegal ametangaza serikali mpya ikiwa na wajumbe kadhaa wa chama kinachoongozwa na aliyekuwa mshirika wake na waziri mkuu aliyemfuta kazi, Ousmane Sonko, aliyeapa kutokuiunga.

Senegal Mbour 2024 |  Bassirou Diomaye Faye & Ousmane Sonko
Marafiki waliogeukana: Rais Bassirou Diomaye Faye wa Senegal (kushoto) na Spika Ousmane Sonko.Picha: Mosa'ab Elshamy/AP Photo/picture alliance

Tangazo la jana la Faye linakuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu amfukuze kazi Sonko, na kulivunja baraza lake la mawaziri kwa kutafautiana juu ya uendeshaji uchumi.

Sonko, ambaye ni mashuhuri zaidi kuliko Faye, alichaguliwa hapo hapo kuwa spika wa bunge na wafuasi wake katika hatua inayoashiria mkwamo mpya wa kisiasa ndani ya taifa hilo la magharibi ya Afrika.

Sonko ndiye kiongozi mkuu wa Pastef, chama alichokianzisha mwaka 2014 na ambacho Faye ni mwanachama wake na kinachohodhi viti 130 kati ya 165 bungeni.

Hapo jana, waziri mkuu mpya, mchumi Ahmadou Al Aminou Mohamed Lo, alitangaza majina ya mawaziri wapya 30, lakini Sonko alisema chama chake hakitajiunga na serikali hiyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW