1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sonko asema mapinduzi ya Guinea Bissau sio halali

28 Novemba 2025

Waziri Mkuu wa Senegal Ousmane Sonko amesema mapinduzi ya wiki hii nchini Guinea-Bissau sio halali na akataka mchakato wa uchaguzi kuruhusiwa kuendelea, hatua inayoongeza sauti ya kikanda dhidi ya mapinduzi hayo.

Senegal Dakar 2024 | waziri Mkuu Ousmane Sonko
Waziri Mkuu wa Senegal Ousmane Sonko akitoa hotuba bungeni mnamo Desemba 27, 2024Picha: Seyllou/AFP

Akijibu maswali kutoka kwa wabunge, Sonko amesema tume ya uchaguzi nchini Guinea Bissau lazima iweze kumtangaza mshindi.

Hapo jana baada ya jeshi kumuapisha Jenerali Horta Nta Na Man kama rais wa mpito atakaeshikilia wadhifa huo kwa kipindi cha mwaka mmoja, kiongozi huyo alisema  mapinduzi hayo yalihitajika ili kuzuia njama ya walanguzi wa dawa za kulevya kudhibiti demokrasia ya nchi hiyo na akaapa kusimamia kipindi hicho cha mpito kilichoanza mara moja.

Umoja wa Ulaya na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Mahmoud Ali Youssouf pia wametoa wito wa kurejeshwa kwa utaratibu wa kikatiba.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW