1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Itikadi kali za mrengo zinatishia demokrasia Ujerumani

9 Novemba 2025

Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ameonya kuwa ongezeko la itikadi kali za mrengo wa kulia na ubaguzi dhidi ya Wayahudi vinazidi kutishia kwa kiasi kikubwa demokrasia nchini humo.

Berlin, 09.11.2025
Rais wa Ujerumani Frank Walter SteinmeierPicha: Maryam Majd/POOL/AFP/Getty Images

Steinmeier amezungumzia kuhusu ongezeko la siasa kali za mrengo wa kulia katika mfumo wa chama kinachopinga wahamiaji  cha Alternative for Germany (AfD), ambacho kilipata asilimia 20.5 ya kura katika uchaguzi mkuu wa Februari na kushika nafasi ya pili.

Ujerumani yaadhimisha miaka 36 tangu kuanguka ukuta wa Berlin

Rais Steinmeier ametoa kauli hiyo katika makazi yake rasmi mjini Berlin wakati Ujerumani inaadhimisha leo miaka 36 tangu kuanguka kwa Ukuta wa Berlin. Tukio hilo lilihitimisha enzi ya utengano na kufungua njia ya kuungana tena kwa iliyokuwa Ujerumani Magharibi na Mashariki.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW