1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Mwakilishi wa Marekani kukutana na Vladimir Putin Urusi

26 Novemba 2025

Ikulu ya Urusi Kremlin, imethibitisha kuwa mwakilishi wa Marekani Steve Witkoff atakutana na Rais wa Urusi, Vladimir Putin wiki ijayo huku Marekani ikiendeleza juhudi za kupata makubaliano ya kuumaliza mzozo wa Ukraine.

Steve Witkoff atakutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Moscow kujadili mpango uliopendekezwa na Rais wa Marekani Donald Trump
Mjumbe Maalumu wa serikali ya Marekani Steve WitkoffPicha: Alexander Drago/UPI Photo/Newscom/picture alliance

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kufanyika wakati Marekani ikiendelea kushinikiza mazungumzo ya usuluhishi kwa ajili ya mpango wa kuumaliza mzozo wa Ukraine. Kremlin imeongeza kuwa, sehemu ya mpango wa sasa wa Marekani zinaleta matumaini, lakini bado kuna vipengele vinavyohitaji mjadala.

EU yasisitiza iko bega kwa bega na Ukraine

Wakati huo huo, Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von Der Leyen amesema chombo chake kipo tayari kuwasilisha nyaraka za kisheria kuhusu matumizi ya mali za Urusi zinazoshikiliwa kutokana na vita vya Ukraine.

Ameyasema hayo katika hotuba yake mbele ya Bunge la Ulaya na kuongeza kuwa Umoja wa Ulaya unaiunga mkono Ukraine katika kila hatua hadi amani itakapopatikana. Von der Leyen amepongeza pia juhudi zinazofanywa na Marekani kuutatua mzozo huo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW