1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroChina

Stoltenberg aitaka China iwajibishwe kwa kuiunga mkono Urusi

18 Juni 2024

Katibu Mkuu wa jumuiya ya kujihami ya NATO Jens Stoltenberg amesema China inapaswa kuwajibishwa iwapo itaendelea na mkondo wake wa kuiunga mkono Urusi.

Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg
Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg akizungumza na waandishi wa habari kabla ya mkutano wa Mawaziri wa Ulinzi wa NATO mjini Brussels, Ubelgiji mnamo Juni 13, 2024.Picha: Dursun Aydemir/Anadolu/picture alliance / Anadolu

Stoltenberg ameeleza kuwa China inajaribu kutimiza malengo mawili kwa wakati mmoja, kwa kuiunga mkono Urusi kwa upande mmoja huku ikijaribu pia kudumisha uhusiano na mataifa ya Magharibi.

Ameishtumu China kwa kuuzidisha mzozo kati ya Urusi na Ukraine kupitia kile maafisa wa Marekani wanachosema kuwa Beijing inaisaidia Urusi kwa kuipa vifaa vya kijeshi.

Soma pia: NATO yajadili utayari wake wa silaha zake za nyuklia

China hata hivyo imetetea uhusiano wake na Moscow na kuzitaja ripoti za Marekani kama upotoshaji.

China imekwenda mbali zaidi na kusema, haitoi msaada wa silaha kwa pande yoyote katika mzozo kati ya Urusi na Ukraine, tofauti na inavyofanya Marekani na washirika wake wa Magharibi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW