1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sudan: Wanajeshi wa kulinda amani wauawa

15 Julai 2013

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshutumu kwa kauli moja shambulizi lililofanywa dhidi ya wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika huko Darfur ambalo lilisababisha vifo vya wanajeshi 7.

Wanajeshi wa Umoja wa Afrika
Wanajeshi wa Umoja wa AfrikaPicha: M. Longari/AFP/Getty Images

Wanajeshi hao waliouawa ni wa Tanzania. Kauli kama hiyo imetolewa na Umoja wa Ulaya ambao umeitaka Sudan kuwachukulia haraka hatua za kisheria waliohusika. Bruce Amani amezungumza na msemaji wa jeshi la Tanzania Kapambala Mgawe ambaye kwanza alianza kwa kumueleza hisia zake kuhusiana na shambulizi hilo na jinsi hali ilivyo kwa sasa. Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Bruce Amani

Mhariri: Yusuf Saumu

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi

Gundua zaidi