Mfalme wa Swaziland ametangaza kwamba nchi yake imebadilishwa jina na sasa inatwa eSwatini. Mfalme Mswati amesema hatua hiyo imechukuliwa ili kuadhimisha miaka 50 tangu nchi hiyo ipate uhuru wake kutoka kwa Waingereza. Jina hilo linamaanisha nchi ndogo iliyoko katikati ya Afrika Kusini na Msumbiji.