1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sydney: Mtuhumiwa wa ugaidi afutiwa mashitaka

27 Julai 2007

Maafisa nchini Australia wameyafuta mashitaka ya ugaidi dhidi ya daktari wa kihindi aliyekamatwa kuhusiana na jaribio lililoshindwa la kuripua bomu lililotengwa garini nchini Uingereza . Dr Mohammed Haneef mwenye umri wa miaka 27, alishitakiwa kwa kusaidia katika njama hiyo kwa kumpa jamaa yake anayeishi Uingereza kadi ya simu yake ya mkononi. Alikua gerezani tangu tarehe 3 mwezi huu, alipokamatwa akijaribu kuondoka Australia kuelekea India.

Waziri wa uhamiaji wa Australia amesema leo kwamba Haneef atabakia gerezani, hadi uamuzi utakapotolewa kuhusu suala la kuhamia kwake nchini humo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW