1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSyria

Syria na Israel kuanza awamu mpya ya mazungumzo

5 Januari 2026

Maafisa wa Israel na Syria wanatajiwa kukutana mjini Paris kuanza tena mazungumzo yaliyoratibiwa na Marekani, huku kukiwa na matumaini ya kufikiwa kwa makubaliano ya usalama kama hatua ya kuondoa mivutano.

Syria Beit Jin 2025 | Uharibifu na vifusi baada ya shambulio la kijeshi la Israel
Uharibifu na vifusi baada ya uvamizi uliofanywa na jeshi la Israel katika kijiji cha Beit Jin, kilichopo katika eneo la Qatana kwenye eneo la mashambani la Damascus kusini mwa Syria mnamo Novemba 28, 2025.Picha: Bakr Al Kasem/Anadolu/picture alliance

Afisa aliyezungumza kwa sharti la kutotambulishwa kwa kuwa hakuwa na ruhusa ya kuzungumza hadharani, ameliambia shirika la habari la AP kwamba ujumbe kutoka Syria utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje Asaad al-Shibani na Mkuu wa Kurugenzi Kuu ya Ujasusi, Hussein Salameh.

Amesema, lengo kuu la Syria kwenye mazungumzo hayo ni kufufua tena makubaliano ya kujitenga ya mwaka 1974 yalioanzisha eneo la ulinzi linalodhibitiwa na Umoja wa Mataifa kusini mwa Syria na kuhakikisha vikosi vya Israel vilivyotwaa udhibiti wa eneo hilo la ulinzi zaidi ya mwaka mmoja uliopita vinaondolewa.

Hata hivyo, si maafisa wa Israel wala msemaji wa ujumbe wa Marekani nchini Syria Tom Barrack walikuwa tayari kuzungumzia hilo, walipoombwa kufanya hivyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW